letras.top
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

letra de interview - rapcha

Loading...

asubuhi flani hang over bwii

nani tena huyu ananipigia saa hii

napapasa kuitafuta simu mpaka naikamata

macho kwenye screen naona jina “gachi b”

we mshezi una balaa hatari

sjui zilikua ni tungi au vijiti walimix wale

uliwaka ukavamia dem wa mtu ukamshika shika

na ukawa unaforce k-mkiss eti palepale
nlijua lazma utani-roast

sjawahi waka vile mpaka ikatokea hadi data zime-lost

mchizi alinitwika ngumi bufff kwenye mdomo yani nkahisi nmepoteza meno yote on the spot

usingeweza kutoboa pale

ilibidi ncheki gap tuch0m-ke tukimbie mbali

nlikudrop kwako ukanambia nkushtue mapema

una interview ya kazi leo katafte ugali

ayaaa nahisi nshachelewa

duhh mchongo bado nusu saa nkichelewa hawatonielewa

umetisha kunishtua acha niwahi chap nkawaskie nikitoka ntadondoka studio

oyеah

haya

mswaki dakika moja, kuoga dakika moja
suruali ya kitambaa imejikunja na iko moja

ila haya yote ningeandaa tangu jana isingеkua kazi fresh nitanyoosha daika moja

naboost simu isinizimikie nkiwa njiani

muda unaenda sana sa inabidi ntoke ndani

navaa chap uber njoo nifate sinza vatcani

sina muda wakuelekeza fata ramani

dakika mbili uber akafika

madevera smart kama wewe mjini ndo wanahitajika

skia nirushe chap posta pale 99 plaza ntakuongeza buku 5 tukiwahi kufika

palepale kwanza dreva kawaka

daah leo ka bahati yani mzee wa lissa nimekunyaka

hivi kwenye ule wimbo ulipigwa kweli?

sioni hata makovu na ile story vipi ishakukuta kweli!??
sasa hapa ndo tutapochelewa

focus yako iwe kwenye kuniwahisha na sio kuongea

mgenilipa kama mnavyonisifia

saivi nsingekua busy kutafuta kazi nisiyoielewa

hii ndo shida ya wasanii bongo

mbele ya camera wapole sana na kujisifia uongo

mnasema mnatupenda mashabiki

ila tunapokutana mnatutreat kama vile tunanuka shombo

na ndo shida ya mashabiki wa bongo

mnapenda tu kupuuzia ukweli na kuamini uongo

mnasahau ka na si ni binadamu kuna muda tuna stress zetu mtuvumilie kidogo

muda unaishia afu bado kuna umbali

nikamlipa dreva nikashuka kwenye gari

psss psss boda niwahishe posta chap tu

zimebaki dakika 5 ufike muda wa interview

mbio mbio mpaka destination

zimebaki dakika mbili tu afu mchiz ndo naingia reception

dada wa mapokezi akafurahi aliponiona

si akataka alete story nkaona ananichoma

nkiwa palepale reception

najibizana huyu sista, haki nimechoshwa na questions

wakaingia watu wawili ndani
yule dada alivyowasalimia ikabidi nkae attention

nageuka nione kuna nani

ndo namuona yule dada ambae jana nilimfata nkamletea uhuni

pembeni yake kaongozana na mumewe alieyataka kunitoa meno na ndio boss wa kampuni

ilinichukua ka nusu sekunde kuk-mbuka ule uzito wa ile ngumi kwenye lile tukio

nkakamata bahasha ya vyeti vyangu kwa makini nkatazama mlango ulipo vvvuuum nkatimua mbio

letras aleatórias

MAIS ACESSADOS

Loading...