letras.top
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

letra de rafaeli - freddy saganda

Loading...

[intro]
woo huu…..
yeah, yeah…

[chorus]
ah, ni namna gani, ah, ni jinsi gani?
tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani, ah, ni jinsi gani?
tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani, ah, ni jinsi gani?
tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani?
ah, ni jinsi gani? (yesu w-ngu)

[verse 1]
ilikuwa jumapili nikamuona rafaeli amekaa juu ya nini’ ni juu ya baiskeli
namuuliza anaenda wapi, kaniambia anaenda ferry, uko ferry ni kwa nani? kwa lile jitu tapeli
sasa utamuona wapi?
atakuwa’ kwenye meli, kwenye meli ndio wapi, ndio huko huko tena
baadae namuona huyo huyo rafaeli anacheza na nani?
na yule dada mary
namuuliza rafaeli’ hapa ndio ferry? anasema’ sio hivyo, mwenzio ni unajua mi nimeharibikiwa na ile baiskeli, nategemea kwenda kule oysterbay
nako huko ntamkuta’ braza mtei, yeye ndo atakaye nipunguzia bei’ ya spea za baiskeli

[chorus]
ah, ni namna gani, ah, ni jinsi gani?
tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani, ah, ni jinsi gani?
tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani?
yesu w-ngu!
ni jinsi gani? (yeleuwi)
ni jinsi gani tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani?
ah, ni jinsi gani?
[verse 2]
kesho yake nikatoka’ moja kwa moja kwa rafaeli, nikamkuta nyumbani ana sikiliza cd ya r.kelly
nikamuuliza rafaeli unaye cd ya makavelli?
akaniambia ana makavelli ya r.kelly na mariah carey
sisi hatuku kaa’ tuka toka moja kwa moja, hao…
mpaka kwenye bar, unaambiwa watu walikuwa wamejaa, ukiangalia nje zime shengamana baiskeli’ na moto-car
basi tukaagiza masanga pale na kitimoto, tukaanza kupata moja baridi, moja moto
wakati tunaendelea eh
kidogo tu
huyo…katokea mzee urassa’ na ile land-cruiser yake new model ya kisasa, power engine 2.4, pulling system ya kisasa, unaambiwa ni automatic kuanzia viti’ hadi vitasa
basi alikuwa na laki tatu mf-koni, akajishika kiunoni, akatuangalia usoni, akatudharau, akaingiza mkono mf-koni, akatoa pesa akaweka pale mezani, kisha akaenda chooni
sisi basi tukaanza kulewa, tukalewa, tukalewa, yesu w-ngu!
tulilewa, tulilewa, tulilewa, tulilewa, wakaongezeka ndugu zetu kutoka sehemu mbalimbali za kilimanjaro;
marangu, machame, uru, kishumundu, kibosho, mwika, vunjo mpaka kiboriloni, unaambiwa tarakea mpaka huku sehemu za rombo, wote pale’ wakawa wamemiminika (wacha bwana!)
massawe alikuwepo
marrealle alikuwepo
shirima alikuwepo
mangi alikuwepo
lema alikuwepo
ndossy alikuwepo
mlei alikuwepo
azei alikuwepo
mama prisca alikuwepo
mama manka alikuwepo
minja alikuwepo
kilua alikuwepo
na huyu mtoto anakaa mtaa wa pili, nani huyu?…
chuwa?
hehe eti chuwa naye alikuwepo…
[chorus]
ah, ni namna gani, ah, ni jinsi gani?
tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani,(yeleuwi!) ni jinsi gani?
tuta win maishani (yesu w-ngu), mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani? ah, ni jinsi gani? tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani?
ah, ni jinsi gani?
kwakweli…

[verse 3]
wakati tunaendelea kupata pale masanga na kitimoto
rafaeli na massawe hao…wakatoka’ sikujua kinachoendelea’ nikajua wanaenda kuruka majoka
kwasababu kulikuwa na mziki wa reggae, charanga, na ule mziki wa kufoka foka
akilini mw-ngu nilikuwa nafikiri kwamba mambo yataenda ya kifanya nini?…
he, yakienda ya kinyooka!
k-mbe huko walipo kwenda walienda ku-kuwachokoza wake za watu wakiwa wameketi, wakaanza kuwashika shika mabegani mpaka zile sehemu zao nyeti
basi waume zao nikaona wamechukia, maneno machafu wakaanza kuwatupia
kinabo wewe!
oi!
muache mke w-ngu kima wewe! unamshikia nini huko!
mara huyu ka-kamtukana mwenzake sijui kamwambia, “fala wewe”, huyu kamrudishia maneno yale na yale; ili mradi tu’ ikawa vurugu mechi
basi wale wanaume nikaona wamebeba mawe’ wakataka wamponde nayo massawe
basi rafaeli akamrukia teke mmoja wao (ti…!)
akamuangusha pale pale, (yesu w-ngu!)
akataka akimbie, ajafika mbali, akakamatwa na nani?
na yule afande chale
asa mi nikamwambia afande chale naomba basi umruhusu huyu rafaeli nyumbani ah-akalale
akaniambia ni lazima kituoni huyu rafaeli leo’ akalale
sasa nikaona sina tena la kufanya
rafaeli ndo huyo tena’ amesha ulowanya (yesu w-ngu!)
kwanza mimi kichwani lager zishanichanganya
ikabidi ningoje nijue kesho kitu gani nitafanya
basi’ maana rafaeli ndio kama ameua, basi pesa zangu zote polisi watakuwa wamechukua (yesu w-ngu, yeleuwi!)
pesa ni maua, maana maua hunyauka vile vile huchanua
ah!
[chorus]
ah, ni namna gani, ah, ni jinsi gani?
tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani, ni jinsi gani?
tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani? ah, ni jinsi gani? tuta win maishani mpaka siku tunasema buriani
ah, ni namna gani? (yesu w-ngu, yeleuwi!)
mura mura mai
ah, ni jinsi gani?
ah, ni namna gani?

[outro]
big up to all the n-ggas from kibosho
n-ggas from marangu
n-ggas from mwika
n-ggas from rombo, moshi mjini, pale’ old moshi and many many places
representing the area
wa-chagaa tupo’ hatupo nyuma kwa hip-hop (tell them!)
yeah…
big up to mama prisca, popote ulipo
big up to mama manka, popote ulipo
i’m telling you, i’m representing this sh-t’ for real
if you dont care’ pack up your bags and luggage and go home
this is how we do, mtatutambua wachagaa mwaka huu…

letras aleatórias

MAIS ACESSADOS

Loading...